Website ni mkusanyiko wa kurasa zilizopo mtandaoni zinazopatikana katika jina moja yani 'domain name'. Kwa Kiswahili website inajulikana kama tovuti. Mfano ni kama facebook.com na millardayo.com
Website huwa zinapatikana katika mtandao. Mara nyingi zinahusu mada fulani kama habari, elimu, biashara au mtandao wa kijamii.
Unaweza kuingia katika website au tovuti kwa kutumia kifaa kitakachokuruhusu kufanya hivyo. Vifaa ni kompyuta, laptop, simu janja au tablet. Ili uweze kuingia pia unahitaji app au software inayoitwa kivinjari (web browser).
Website yenye machapisho ya mara kwa mara huitwa blog

Andika Comment:
Comments 0 :
Acha comment yako hapa